27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Mchambuzi atimuliwa studio kwa kauli ya ubaguzi dhidi ya Lukaku

MILAN, ITALIA

Kituo cha Televisheni nchini Italia, kimemfukuza kazi mchambuzi wa soka, Luciano Passirani kwa maoni ya ubaguzi wa rangi juu ya straika wa timu ya Inter Milan, Romelu Lukaku ambaye aliwahi kucheza Manchester United.

Passirani akizungumza kwenye kituo cha televisheni kama mchambuzi alitamka  maneno ya kibaguzi dhidi ya straika huyo raia wa Ubelgiji, kwamba huwezi kuchukua mpira mchezaji huyo akiwa anaumiliki na ili uweze kuuchukua ni lazima umrushie ndizi 10 ili aachie mpira huo.

Baada ya kauli hiyo, Passirani (80) aliomba msamaha lakini alikuwa amechelewa kwani mwongozaji wa kipindi hicho, Fabio Ravezzani alichukua hatua ya kumfukuza kazi mchambuzi huyo akiwa studio.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles