23.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Mbunge atishia kuvua nguo bungeni kisa maji

Arodia Peter, Dodoma

Mbunge wa Nsimbo, Richard Mbogo (CCM), ametishia kuvua nguo bungeni ikibidi ili yapatikane maji safi na salama kwenye jimbo lake.

Mbogo ametishia hivyo wakati akichangia mjadala wa Wizara ya Maji bungeni leo Mei 3, ambapo amesema suala la maji halina mbadala hivyo Serikali itatue tatizo hilo jimboni mwake.

Amesema kama ilivyokuwa kwa mtumishi wa Mungu, Ibrahimu, alikuwa tayari kumchinja mwanawe, lakini baadaye Mungu alimpatia mwanakondoo wa kuchinja, mwanawe akanusurika.

“Mheshimiwa mwenyekiti, suala la maji safi na salama si la mzaha, ikibidi niko tayari kuvua nguo hapa bungeni ili nipate suluhisho la upatikanaji wa maji Nsimbo.

“Kama kuonyesha niko ‘serious’ kwa jambo hili niko tayari kufanya lolote, kama kuna jambo mnaweza kufanya mtuambie tufanye, tozo hii ya Sh. 50 ni muhimu sana,” amesema Mbogo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles