25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Mbunge adai ukosefu wa maji unateteresha ndoa

Arodia Peter, Dodoma

Mbunge wa Handeni Vijijini, Mboni Mhita (CCM), amesema ndoa za wanawake wa jimbo hilo zimetetereka kwa sababu wanaamka alfajiri kwenda kuchota maji.

Akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Maji bungeni leo Mei 2, Mboni amesema badala ya wanawake kuhudumia ndoa zao muda huo hutoka kwenda kusaka maji na hivyo kuhatarisha ndoa zao.

“Ndoa nyingi za wanawake wa Handeni Vijijini ziko hatarini wanaamka alfajiri na kushindwa uaminifu, wengine ndoa zao wamezikosa kwa sababu ya kudamka muda huo kwenda kusaka maji na wakati mwingine hurudi bila maji,” amesema Mbunge huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles