26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Mboya ashinda kura za maoni Moshi Mjini

Upendo Mosha, Moshi

Aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Moshi, Raymond Mboya ameshinda kura za maoni za kuomba kuteuliwa kuwania ubunge wa Jimbo la Moshi Mjini kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Mboya amechaguliwa na wajumbe wa chama hicho wa Mkutano Mkuu wa wilaya ya Moshi Mjini kwa kura 107 ambapo ni sawa na asilimia 70.9.

Akitangaza matokeo hayo msimamizi wa uchaguzi huo, Ephata Nanyaro, alisema Mboya amekuwa mshindi katika uchaguzi huo na anategemewa kupeperusha bendera ya Chadema katika Jimbo la Moshi Mjini.

Aidha alisema wagombea wenza katika uchaguzi huo Ni, Antony Ndewawio  ambaye amepata kura kura 06 sawa na asilimia 3.6, Colince Mayuta  kura 10 sawa na asilimia 6.0Michael Kilawila kura 32 sawa na asilimia 19.4.

Akitoa shukrani zake kwa wajumbe hao, Raymond Mboya alisema amepewa jukumu kubwa la wananchi wa Moshi ya kuwaletea maendeleo na kwamba  atakuwa muaminifu katika shughuli zake zote za kisiasa pasipo kununuliwa.

“Maendeleo yanayoonekana kama reli, barabara na maeneo mengine yanamuhusu mheshimiwa rais hivyo maendeleo yaliopo hapa Moshi Mjini ikiwemo ujenzi wa stendi ya kisasa hapa yananihusu mimi na bado naahidi maendeleo makubwa zaidi, “alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles