23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Mbowe: sitaondoka Chadema kwa shinikizo la CCM

Anna Potinus, Dar es Salaam



Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Freeman Mbowe, amesema hataondoka katika nafasi hiyo kwa shinikizo la wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) isipokuwa wanachama wa chama hicho wakimtaka aondoke ataondoka.

Mbowe ameyasema hayo leo Jumatano Septemba 19, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, ambapo amezungumzia kilichotokea kwenye uchaguzi mdogo wa marudio uliofanyika hivi karibuni na kuelezea msimamo wa chama hicho.

“Hii kazi si nyepesi kama mnavyofikiria ni ya ujasiri wala mtu asifikirie kuna faida kuwa Mwenyekiti wa Chadema huu ni utume, hii kazi ina msalaba ambao sio kila mtu anaweza akaubeba, nimepewa mamlaka na wanachama wangu wakinitaka niondoke hata kesho nitaondoka lakini nikiambiwa na watu walioko CCM siondoki,” amesema.

Pamoja na mambo mengine, Mbowe amesema kelele zinazopigwa na CCM kuhusu wanaohama katika chama chao hazitawaondoa katika reli na kwamba kukimbia kwao hakutawafanya washindwe kwenda mbele

“Kila anapoondoka diwani mmoja kuna wanachama maelfu wanaingia Chadema, wale ambao wana moyo mwepesi wameshindwa kukabiliana na hizi siasa zenye changamoto tunawatakia heri huko wanakokwenda sisi tutaendelea maana wako wanachama wengine wengi tutawaibua utakapofika uchaguzi mwingine ujao”, amesema

Aidha, amesema wanaofikiri kuwa kazi yake ni nyepesi wanakosea na kwamba CCM wasitarajie kuwa ataondoka kutokana na kelele wanazopiga kwani mamlaka hayo alipewa na wanachama wake.

 

 

 

- Advertisement -

Related Articles

1 COMMENT

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles