24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

MBEO AMSAFISHA MBATIA MALI ZA CHAMA

 

Na ESTHER MNYIKA

-DAR ES SALAAM

CHAMA cha NCCR –Mageuzi kimesema hakuna kiongozi  yeyote mwenye mamlaka ya kuuza au kununua  mali za chama bila kupata kibali kutoka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA).

Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya aliyewahi kuwa Mkuu wa Idara ya Kampeni, Faustine Sungura  kuwataka Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia, Katibu Mkuu wake, Martin Danda  na Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini, Mohamed Tibanyendera  kujiuzulu ndani ya siku tatu kutokana na tuhuma mbalimbali zikiwamo ubadhirifu wa fedha na kutaka kukiua chama hicho.  

Ofisa Habari wa chama hicho, Florian Mbeo amesema kwa mujibu wa katiba ya chama  hicho Ibara ya 27 na Ibara ndogo ya 7, kifungu A na B usimamizi wa mali zote za  chama zinazohamishika  na zisizohamishika zipo chini ya uangalizi wa  Baraza la Wadhamini.

Amesema wanachama wanapaswa kufuata taratibu zilizowekwa na katiba na kanuni za chama katika kuwasilisha taarifa zao  kwenye mamlaka stahiki za chama.

“Kwa hiyo Mbatia na wenzake hawana mamlaka ya kuuza mali za  chama na ili waweze  kuuza au kununua lazima wapate kibali  kutoka RITA, na baraza ndio linalo tambulika na RITA na si viongozi, jambo ambalo halikufanyika,” amesema Mbeo

Amesema suala kama hilo lilishatolewa ufafanuzi Desemba mwaka jana, baada ya taarifa kusambaa kwenye mitandao kuwa baadhi ya viongozi wanabinafsisha mali hizo, ukweli ni kwamba hakuna mali yoyote  ya chama iliyotwaliwa binafsi na mwenyekiti wa au kiongozi yeyote kutoka lakini pia  anayo haki ya kununua, kumiliki na kutumia mali yoyote  ambayo amepata kihalali kwa jitihada zake mwenyewe.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles