26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Mawaziri kutoa ripoti ya utekelezaji kila mwezi

Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO), Hassan Abas
Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO), Hassan Abas

NA ESTHER MNYIKA – DAR ES SALAAM

SERIKALI imesema kuanzia sasa mawaziri wote wanatakiwa kutoa taarifa ya utekelezaji wa vipaumbele vya bajeti kwa kila mwezi kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO), Hassan Abas, alisema hiyo ni miongoni mwa mikakati ya Serikali katika kuboresha mawasiliano baina yake na wananchi kwa kuwapatia taarifa za utekelezaji wa ahadi zake.

“Lengo kubwa ni kujua vipaumbele vya  bajeti zao ni vipi na namna ya kutekelezwa, mafanikio na changamoto wanazokabiliana nazo katika utekelezaji,” alisema Abbas na kuongeza:

“Kila mwezi waziri atawasilisha taarifa yake popote pale atakapokuwa kupitia vyombo mbalimbali hususani vipindi maalumu vilivyopo kwenye runinga, redio  na kufanya mkutano.”

“Mkakati huo utaanza Agosti 25 mwaka  huu, ratiba ipo tayari  na taarifa hizo za mawaziri zitapelekwa kwenye mifumo ya ndani ya Serikali.”

Alitaja mkakati mwingine kuwa ni wa Idara ya Habari (Maelezo) kueleza kwa umma kila mara na haraka iwezekanavyo utekelezaji wa sekta zote katika ngazi ya taifa.

Aidha, alisema katika kutekeleza hayo  wiki ijayo ataanza kufanya ziara ya kushtukiza  katika vyombo vya habari vyote nchini kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari.

Alisema atafanya mazungumzo na taasisi  mbalimbali katika kutafuta fursa na mafunzo ndani na nje ya nchi kwa ajili ya waandishi wa habari.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles