Na JENNIFER ULLEMBO – DAR ES SALAAM
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Maua Sama, amefunguka na kusema kuwa haikuwa kazi rahisi kuandaa video ya wimbo wake mpya wa Amen.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Maua alisema ilimchukua takribani saa kadhaa kutengeneza kila kipande kilichopo ndani ya wimbo huo mpya aliomshirikisha Bernad Paul ‘Ben Paul’.
“Kufanya video si kazi rahisi kama wenzetu wanavyofikiria, ukweli nimepata tabu sana katika video yangu ya Amen, kuna baadhi ya vitu vilikuwa ni vigumu kuvifanya kwa harakaharaka,” alisema Maua.
Alisema ana imani wimbo na video ya Amen utapokelewa vema na mashabiki wake ambao wamekuwa wakitamani kumuona akifanya kazi nzuri zaidi zitakazoweza kumsaidia kukuza muziki wake.