27 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Maswali kumi sumu mwilini mwa Mangula

Mwandishi Wetu -Dar es salaam

KAULI ya Jeshi la Polisi kwamba Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Philip Mangula alipewa sumu, imeacha maswali mengi na mjadala mkubwa miongoni mwa jamii.

Februari 28, mwaka huu, Mangula alidondoka ghafla katika ofisi ndogo za CCM Lumumba mara baada ya kumaliza kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichokuwa kikijadili masuala mbalimbali, ikiwamo adhabu kwa wanachama watatu waliokuwa na tuhuma za ukiukwaji wa maadili ndani ya chama hicho.

Katika kikao hicho, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, alivuliwa uanachama kwa tuhuma za ukiukwaji wa maadili kwa mujibu wa katiba ya chama hicho na kanuni ya maadili na uongozi.

Tuhuma hizo pia zilikuwa zikiwakabili makatibu wakuu wastaafu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana ambaye atakuwa chini ya uangalizi kwa miezi 18 na Yusuf Makamba aliyesamehewa makosa yake.

Akizungumza jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, alisema kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, wamebaini ndani ya mwili wa Mangula kulipatikana sumu.

“Machi 2 tulipokea taarifa kutoka uongozi wa CCM kuhusu kuwekewa sumu Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Mangula. Katika taarifa hiyo tulielezwa kwamba Mangula alipelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili na kulazwa chumba cha uangalizi maalumu (ICU).

“Uchunguzi kuhusu tuhuma ya sumu hiyo ilivyoingia mwilini upelelezi bado unaendelea. Jeshi la Polisi litachukua hatua kali kwa mtu yeyote atakayebainika kupanga, kuratibu au kusimamia utekelezaji wa uhalifu huo.

“Haitajalisha awe ni mwanafamilia, awe ni mtu kutoka ndani ya CCM au vyama vingine vya siasa, mwananchi wa kawaida, awe ndani au nje ya nchi, awe serikalini au taasisi yoyote hatua kali zitachukuliwa,” alisema Mambosasa.

Aliwataka wananchi wajiepushe na vitendo hivyo kwani si tu vya kinyama, bali pia vinalenga kukiuka sheria za nchi.

MASWALI KUMI TATA

Kutokana na uzito wa tukio hilo bado limezua sintofahamu katika jamii, huku kukiibuka maswali ambayo hadi sasa bado yamekosa majibu na kusubiri taarifa ya uchunguzi wa Jeshi la Polisi.

Baadhi ya maswali hayo ambayo jamii inahitaji kujua majibu yake ni kwamba Mangula alikuwa wapi baada ya kutoka nyumbani kwake.

Je, aliamkia wapi? Kifungua kimya gani alipata? Usafiri gani alitumia kwa siku hiyo kabla ya kuanguka? Je, alisalimiana na nani? Je, ofisini aliingia saa ngapi na alikutana na nani? Je ni nani alimuhudumia kupata kifungua kinywa ? Je wakati wa kikao alikula na kunywa? Je, alihudumiwaje? Na mfumo wa huduma ulikuwaje?

Pamoja na hayo bado Watanzania wanasubiri na kutaka kujua maendeleo ya afya yake.

JPM ALIVYOMJULIA HALI

Februari 29, mwaka huu, Rais Dk. John Magufuli alimtembelea na kumjulia hali Mangula ambaye alikuwa amelazwa katika chumba cha uangalizi maalumu Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Rais, Ikulu, Gerson Msingwa, Mangula aliugua ghafla na kisha kukimbizwa hospitali kwa matibabu.

Kwa mujibu wa video za Ikulu, Magufuli alionekana akimwombea Mangula kupona kwa haraka.

“Utapona na Mungu atakusimamia utarejea katika majukumu yako, nilikuona jana (Februari 28) umeanguka,  ilitushtua,” alisema Rais Magufuli huku Mangula akisema “sijui niliangukaje.”

Hata hivyo Rais Magufuli, alisema kuwa hawezi kujua kwani wanamkabidhi Mungu ambaye atamsimamia siku zote kwa sababu wanadamu wanalindwa na Mungu ambaye huwapenda sana.

Rais Magufuli alimwomba Mangula kufanya ibada hospitalini hapo na alifanya hivyo.

VIONGOZI NA SUMU

Novemba 12, 2019 Rais Magufuli alisema wakati akiwa Naibu Waziri wa Ujenzi katika Serikali ya awamu ya tatu, alinyweshwa sumu kutokana na utendaji wake wa kazi.

Alitoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa kitabu cha Rais mstaafu Benjamin Mkapa kilichoelezea maisha yake.

“Tulipofanya kazi vizuri kwenye kujenga barabara, mzee Mkapa alifurahi sana, akatamka kwamba mimi ni askari wake wa mwavuli namba moja, ameligusia hili kwenye ukurasa wa 107 wa kitabu chake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles