30.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Marhox aibuka na Kimambo kwenye Sukari

Toronto, Canada

Msanii anayekuja kwa kasi kutoka nchini Canada, Marhox, ameibuka kivingine na wimbo Sukari uliotengenezwa na prodyuza nyota Bongo, Kimambo.

Akizungumza na www.mtanzania.co.tz Marhox amesema ana nyimbo nyingi ambazo amefanya na watayarishaji wakubwa hapa nchini Tanzania, hivyo mashabiki waendelee kumpa sapoti ili awape burudani.

“Nimefanya wimbo kwa prodyuza Kimambo kisha nikapitia Dubai nikafanya hivyo video nikampa Director Joma wa Tanzania aihariri, wimbo nimeimba kwa Kifaransa na Kiswahiliki ufupi ni wimbo mzuri unaozungumzia mapenzi kwani ni Mnamke mtamu kama sukari, mwonekano na mavazi yake yananitamanisha.

Naamini itafanya vizuri kwenye Redio na Tv pia chaneli yangu ya mtandao wa Youtube na mashabiki wataipenda.

“Ninazo nyimbo nyingi sana nimefanya na watayarishaji wengi kama Man Walter pia kuna video nimetoka kumalizia na Lucca Swahili kwa hiyo mashabiki wakae mkao wa kula,” amesema Marhox mwenye asili ya Kongo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles