24.1 C
Dar es Salaam
Sunday, September 8, 2024

Contact us: [email protected]

Marekani mezani na Taliban

Doha, Qatar

KATIKA kikao kilichozikutanisha Marekani na Taliban huko Qatar, taifa hilo lenye nguvu ya kiuchumi duniani limekubali kusambaza misaada ya kibinadamu nchini Afghanistan.

Pande mbili hizo zimekaa mezani kwa mara ya kwanza tangu Taliban ilipoingia madarakani Agosti, mwaka huu, hatua hiyo ikija baada ya Marekani kuondosha wanajeshi wake Afghanistan.

Mbali ya ‘ishu’ ya misaada, pia mazungumzo yao yalijadili namna Afghanistan itakavyolindwa dhidi ya vikundi vya kigaidi vilivyoko ndani ya nchi hiyo.

Kwa upande wao, maafisa wa Marekani waliyataja mazungumzo kwenda kiweledi, huku wakisisitiza kuwa ni zamu ya Taliban kuonesha kwa vitendo dhamira yao ya kutelekeza yale yaliyojadiliwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
589,000SubscribersSubscribe

Latest Articles