23.3 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

MAREKANI: KOREA KASKAZINI ILIKUSUDIA KUFANYA UCHOKOZI

Marekani imesema Korea Kaskazini ilikuwa na nia fulani ilipotekeleza jaribio la kombora ambalo lilifeli mwishoni mwa wiki.

Waziri wa Ulinzi James Mattis amesema jaribio hilo lilikuwa la kutojali na kwamba Marekani inafanya kazi kwa karibu na China kukabiliana na Korea Kaskazini.

Amesema Korea Kaskazini ilifanya hivyo ikikusudia kufanya uchokozi fulani.

Marekani ilisema kombora hilo la Korea Kaskazini lilipuka muda mfupi baada ya kurushwa angani.

Pyongyang imesema inaweza kuwa ikifanyia majaribio makombora kila wiki na pia ikaonya kwamba kutatokea "vita kamili" iwapo Marekani itaichukulia hatua za kijeshi.

"Iwapo Marekani wanapanga kutushambulia, tutajibu kwa shambulio la nyuklia kwa mtindo na njia yetu wenyewe," alisisitiza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Korea Kaskazini, Han Song-ryol

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles