27.9 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Mapera husaidia kurutubisha mayai ya uzazi

pera

Na HERIETH FAUSTINE,DAR ES SALAAM

MAPERA ni matunda yanayopatikana kwa wingi licha ya kutopendwa na watu wengi kutokana na ugumu wake wakati wa kuyatafuna pamoja na kuwa na mbegu mbegu nyingi.

Mapera ni miongoni mwa matunda yenye kiwango kizuri cha vitamin C pamoja na vitamin A na inaelezwa kuwa kiwango cha vitamin C kinachopatikana  ndani ya mapera ni sawa na mara nne ya kiwango cha vitamin hiyo inayopatikana kwenye machungwa na maembe.

Kama yalivyo matunda mengine kuwa na faida mbalimbali katika mwili wa binadamu, mapera nayo ni miongoni mwa matunda hayo kutokana na kuwa faida nyingi ikiwamo kusaidia kurutubisha mayai ya uzazi kwa kuwa yana madini yaitwayo Folate.

Pia yana uwezo wa kuzuia ugonjwa wa kisukari  kutokana na wingi wa fibre ambayo husaidia kupunguza kiasi cha sukari katika damu, vile vile husaidia kusafisha mfumo kwa usahihi.

Kwa mujibu wa utafiti uliowahi kuchapishwa na Jarida la Journal of Human Hypertension mwaka 1993, mapera yanaweza kupunguza kiwango cha msukumo mkubwa wa damu ndani ya mwili, hii ni kwa sababu matunda hayo kuwa na madini ya potassium na vitamin C ambayo husaidia kuweka sawa msukumo wa damu ndani ya mwili.

Pia majani ya mpera yanapoandaliwa kama chai yaani yakichemshwa husaidia kuondoa sumu mwilini, jambo ambalo husaidia kulinda afya ya moyo wako.

Pia husaidia wale wenye tatizo la kuharisha hii ni kwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2008 uliochapishwa kwenye Jarida the Revista do Instituto de Medicina Tropical de São Paulo, ambao walieleza kwamba majani hayo ya mapera yanauwezo wa kuzuia vimelea vya staphylococcus aureus ambavyo huchangia tatizo la kuhara.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles