26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Manchester United Wamepigwa tena

manchester-united-vs-watfordWatford, England

TIMU ya Manchester United jana  ilifungwa  mabao 3-1 dhidi ya  Watford katika mchezo wa Ligi Kuu England, uliochezwa Uwanja wa  Vicarage, jijini Watford.

Mchezo huo  ulishuhudiwa kwa Kocha wa  timu ya Manchester United, Jose Mourinho,  kupoteza mchezo wa tatu  mfululizo, ikiwa  mara ya kwanza tangu mwaka 2006 alipokuwa akifundisha  timu ya Chelsea.

Mashabiki zaidi ya 21,118  waliokuwapo katika mchezo huo, walishuhudia Watford kupata bao la kuongoza dakika ya  32 kupitia kwa  Etienne Capoue.

Kipindi cha kwanza kilimalizika huku  Manchester United  wakiwa nyuma bao 1-0 licha ya  kulishambulia lango la wapinzani wao mara kwa mara.

MShambuliaji wa  United, Marcus Rashford,  alifanikiwa kupata bao la kusawazisha  dakika ya  61  kipindi cha pili, hata hivyo Watford   waliongeza bao la pili kupitia kwa Juan Zuniga dakika 82 na kuchangia ushindi huo  wa kihistoria, baada ya miaka 30 tangu walipowafunga wapinzani wao.

United  waliongeza bao la  tatu kwa mkwaju wa penalti  dakika ya nne ya nyongeza baada ya dakika 90 kumalizika kupitia  kwa Troy Deeney baada ya  Marouane Fellaini kumfanyia   madhambi  Juan Zuniga.

Mchezo  huo ulimalizika kwa United  kufungwa  jumla ya mabao 3-1, ukiwa ni mchezo wa pili wa ligi kuu kupoteza baada ya kufungwa dhidi ya Manchester City mabao 2-1.

United  pia ilifungwa bao 1-0 katika mchezo wa  ligi ya Europa  dhidi ya  Feyenoord na kufanya Maourinho kupoteza jumla ya michezo mitatu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles