27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Mamia ya wanachama CUF Tanga wahamia ACT-Wazalendo

Oscar Assenga, Tanga

Wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) jijini Tanga, kutoka kata 27 na matawi 96, wamemfuata aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif, ACT- Wazalendo na kukabidhiwa kadi za uanachama.

Wakati wanachama hao wakifanya uamuzi huo, leo Jumanne Machi 19, jijini Dar es Salaam, Maalim Seif amekabidhiwa rasmi kadi namba moja ya ACT-Wazalendo iliyolipiwa ada ya miaka 10.

Wanachama hao pia, wamechoma kadi zao za zamani na bendera za CUF, kuashiria kwamba wamejivua uanachama wa chama hicho na sasa wao ni rasmi wanachama wa ACT-Wazalendo.

Wamesema wameamua kumuunga mkono maalimu Seif kujiunga ACT Wazalendo kwani ndio chama makini kinachoweza kuwafikisha kwenye azma yao ya kuiondoa CCM madarakani.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles