31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Mamia warudi CCM Monduli

Mwandishi Wetu, Monduli

Mamia ya wananchi wilayani Monduli, mkoani Manyara akiwamo aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Longido Onesmo Ole Nangole, wamerejea Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuungana na Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa.

Wanachama hao walitumia fursa ya mkutano wa kumkaribisha Lowassa uliofanyika Monduli leo Jumamosi Machi 9, wakati akipokewa na wanachama wa chama hicho.

Katika mkutano huo, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole, alitumia fursa hiyo kuwalisha kiapo wanachama waliorudi CCM wakiongozwa na Lowassa.

Polepole amesema kanuni za Chama hicho zinawataka wanachama wengine wanaotaka kurudi kuandika barua ngazi ya Tawi ili waweze kujadiliwa kama alivyofanya Lowassa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles