31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Malaika atamani kolabo na Chege

Glory Mlay – Dar es Salaam

MSANII wa muziki nchini, Diana Exavery ‘Malaika’ amesema anatamani kufanya kolabo na msanii Said Hassan maarufu ka jina la Chege.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Malaika alisema, Chege amekuwa msaada mkubwa kwake kumsapoti kwenye shughuli zake za muziki hivyo anatamani kufanya naye kazi.

“Chege ni baba yangu kimuziki kwa sababu ni mzoefu na nilimkuta na amekuwa mstari wa mbele kunipa ushauri, kunitia moyo na kunisapoti, hivyo mambo yakiwa sawa nitakuja kufanya naye kazi,” alisema.

Alisema kwa sasa yupo kimya kutokana na shughuli mbalimbali za kijamii anazozifanya hivyo ikifika muda atarudi rasmi kwenye muziki.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles