26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Mahakamani kwa kumuua mtoto wake

Aveline Kitomary, Dar es Salaam

Mwanamke mmoja Mkazi wa Mburahati NHC, Angelina Joseph (23), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni kwa kosa la kumuua mtoto wake.

Mwendesha mashtaka wa Serikali, Ramadhan Mkimbo, amedai hayo leo Jumatano Desemba 19, mbele ya Hakimu Frank Moshi.

Amedai Novemba 5 mwaka huu, jijini Dar es Salaam, mshtakiwa kwa makusudi alisababisha kifo cha mtoto wake mchanga wa siku mbili.

Mshtakiwa hakutakiwa kujibu tuhuma hizo kutokana na Mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi hiyo na kurudishwa rumande hadi Desemba 21, mwaka huu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles