25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Mahakama: Uingereza inaweza kubatilisha uamuzi wa Brexit

BRUISSELS, UBELGIJI

MAHAKAMA ya Sheria ya Ulaya (ECJ) jana imetoa uamuzi kuwa Serikali ya Uingereza inaweza kuubatilisha uamuzi wake wa kujiondoa umojani humo (Brexit) bila ya kutafuta ridhaa ya nchi nyingine wanachama.

Uamuzi huo umetolewa siku moja kabla ya wabunge waUingereza hawajapiga kura kuamua kama wayaunge mkono makubaliano ya Brexit yaliyofikiwa kati ya Uingereza na Umoja wa Ulaya au la.

 Uamuzi wa ECJ unaoenekana kama ushindi kwa watu wanaotaka kura nyingine ya maoni ifanyike Uingereza itakayoizuia nchi hiyo kuondoka EU mwakani.

Waziri wa Mazingira wa Uingereza, Michael Gove amesema mpango wa Waziri Mkuu Theresa May utapigiwa kura hiyo leo, kama ilivyopangwa.

Hata hivyo, taarifa zilizojitokeza baadaye jioni zinaonesha kuwa huenda mchakato huo wa kura bungeni unaweza usiwepo leo hadi itakapotangazwa tena.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles