Na Mwandishi Wetu-DODOMA
RAIS Dk. John Magufuli ametengua uteuzi na kumsimamisha kazi Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Uledi Mussa.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, ilieleza kwamba kutenguliwa kwa uteuzi na kusimamishwa kazi kwa Uledi kunaanzia jana.
Kwamba hatua hiyo imechukuliwa ili kupisha uchunguzi zaidi dhidi ya Uledi kutokana na kutozingatiwa kwa taratibu zinazotakiwa katika kushughulikia masuala ya uwekezaji.