23.3 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

MAGAIDI WAUA SABA UINGEREZA

LONDON, UINGEREZA



WATU saba wameuawa na wengine zaidi ya 30 wanatibiwa hospitali baada ya watu wanaoaminika kuwa magaidi kuendesha gari na kuwagonga wapita njia kisha kuwachoma visu watu waliokuwa baa usiku wa kuamkia jana.
Washambuliaji watatu ambao  walikuwa  wamevalia  mikanda  ya  bandia  ya  milipuko, pia walipigwa  risasi na  polisi  na  kufa. Polisi mjini hapa wamesema.


"Katika  wakati  huu, tunaamini watu  saba  wameuawa  pamoja  na  washambuliaji watatu waliopigwa  risasi  na  polisi," alisema  Kamishna  Msaidizi  wa Polisi Mark Rowley  ambae pia  ni  mkuu  wa  kitengo  cha  kupambana  na  ugaidi.


Washukiwa  waliwagonga  wapita  njia  katika  daraja  la  London  kabla  ya  kuwashambulia watu waliokuwa baa za  karibu  na  migahawa, Rowley  alisema. 


Polisi  wenye  silaha waliwapiga  risasi  washambuliaji  watatu  katika  muda  wa  dakika  nane   baada  ya kupokea  simu ya  kwanza kuhusu   mashambulio.


Watu walioshuhudia  waliliambia  gazeti  la  Guardian kuwa waliwaona  watu  wawili wakiwachoma visu  watu  nje  ya  mgahawa  maarufu  wa  Roast  katika  Soko  la  Borough. 


“Walikuwa  wakiwachoma  visu  watu, tulikuwa  tunapiga  kelele ‘acha, acha’  na  watu walikuwa  wakiwatupia  viti kabla ya polisi kuwasili na kuwapiga risasi,” shuhuda mmoja alisema.


Waziri  Mkuu wa Uingereza, Theresa  May  ameliita  shambulio  hilo  kuwa ‘tukio la kigaidi’ na  alieleza ‘shukrani  zake nyingi’ kwa  polisi  na  huduma  za  dharura. 


Rais wa Marekani, Donald Trump, amempigia  simu  May  na  kumpa rambi rambi  zake  kufuatia tukio  hilo.
Aidha viongozi mbalimbali duniani akiwamo Waziri  Mkuu  wa  Canada  Justin Trudeau, Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, Kiongozi wa Ujerumani, Angela Merkel wamelaani vikali tukio hilo.


Shambulio hilo ambalo limetokea ikiwa ni wiki kadhaa tu baada ya watu 22 kuuawa baada ya mtu mmoja wa kujitoa mhanga kujilipua ndani ya ukumbi wa burudani mjini Manchester.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles