27.9 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Mafundi umeme watakiwa kuwa na leseni

Na Sheila  Katikula, Mwanza

Mafundi umeme wametakiwa kujisajili  na kupewa  leseni na Mamlaka ya Udhibiti ya Huduma za Nishati na Maji  (EWURA) ili kuzuia  ajali za moto zinazosababisha vifo na uhalibifu wa  mali sanjari na kuepuka vishoka.

Akizungumza na www.mtanzania.co.tz , Meneja wa Mamlaka  ya Udhibiti ya Huduma za Nishati na Maji ( EWURA) Kanda ya Ziwa, George Mhina,  alisema lengo la utoaji wa leseni  za kuunganishia  mifumo ya umeme  kwa mafundi hao  itasaidia kila mtu kufikiwa na nishati hiyo kwa uhakikika na usalama.

Alisema hadi sasa zaidi ya mafundi 3,500 wamesajiliwa kwa nchi nzima na kupewa leseni ili waweze kufanya kazi kwa uhakika kwani kufanya kazi bila  leseni ni kosa na adhabu zitachukuliwa ikiwemo  kifungo cha miaka mitano au faini isiyozidi sh milioni 10 au adhabu zote mbili kwa pamoja.

“Maombi ya leseni  hufanywa  mtandaoni kupitia mfumo wa Lois  katika tovuti ya mamlaka  hiyo  zinatolewa   kulingana na sifa  za mwombaji  ambapo daraja A ni fundi mwenye uwezo wa kufanya kazi  zote za ufungaji na usambazaji umeme, daraja B  ufungaji umeme msongo wa  kati  hadi  volti 33,000.

“Kwa daraja C  fundi anakuwa na leseni ya ufungaji  umeme  usiozidi  volti 400, na mwombaji anapaswa  kuwa na nakala ya picha ya rangi ya bluu  (pasipoti), kuambatanisha Wasifu (CV)na nakala ya  vyeti vya elimu ya ufungaji   umeme  hati ya kusafiria, kitambulisho cha taifa,” alisema.

Hata hivyo Mbina amewataka wananchi kuhakikisha wanaweka utaratibu wa kukagua nyaya za umeme kwenye nyumba zao ili kuweza kubaini kama zimechubuka  na kuzibadilisha  ili kuepuka majanga ya moto. 

“Hivi karibuni tumeshuhudia shule zikiungua na kusababisha  vifo na mali kuteketea, sheria inasema  kila baada ya mwaka  mmoja  unapaswa kuangalia nyaya kama zipo vizuri kwenye nyumba na kumbi za starehe na kwenye shule kila baada ya miaka mitano.

“Kwa viwandani kila baada ya miaka mitatu inashauriwa zoezi hilo ili kuepuka na changamoto hiyo ni vema kuweka utaratibu wa kukagua nyaya kama sheria zinavyosema,” alisema Mhina.

Mhina alisema kwa mjibu wa kanuni zilizowekwa na mamlaka hiyo wananchi hawapaswi kuwapa kazi ya kufunga umeme kwenye nyumba zao na viwanda kwa mafundi ambao hawana leseni ya mamlaka hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles