PARIS, Ufaransa
WATU wapatao 1,726 walikamatwa na polisi kufuatia maandamano yaliyoikumba nchi hii wiki iliyopita katika maeneo mbalimbali kupinga ongezeko la kodi katika bidhaa mbalimbali hususan za mafuta.
Taarifa hiyo metolewa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Christophe Castaner na akasema waandamanaji 1,220 waliwekwa rumande na wengine 619 wamshafunguliwa mashtaka.
Waziri huyo alisema waandamanaji wengi walikutwa na silaha ingwa mawakili wao wanadai kuwa hawakuwa na vitu kama bali waliandamana kuonesha hisia zaoa kali na wala hawakufanya vurugu zozote.
Waziri huyo alisema kuwa wengi wa waandamanaji ambao wanawashikilia mahabusu wanatuhumiwa kufanya vurugu ama kuhamasisha uharifu.
Jumamosi hiyo ilishuhudiwa maandamano mengine ya nne yanayowahusisha watu wanaohitwa vizibao vya njano ambao wanapinga kuongezwa kwa bei ya mafuta, kodi na ghrama za maisha.
Katika jiji hili la Paris, Lille, Lyon, Marseille, Nantes na Toulouse waandamanaji hao walipambana na polisi na kati yao 135 walijruhiwa mjini hapa.
Maandamano hayo yalianza baada ya Novemba 17 mwaka huu serikali kutangaza kuwa bei yha mafuta ya petroli na dizeli nchini itapanda kuanzia Januari mosi mwakani senti Euro 3 kwa petrol na senti Euro 6.5 kwa dizeli.