31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Madiwani waomba wabunge kuwatafutia gari la kubebea wagonjwa

FLORENCE SANAWA-MTWARA

Madiwani wa Manispaa ya Mtwara Mikindani, wamewaomba wabunge kuwasaidia kupata gari la wagonjwa ili kuweza kukabiliana na changamoto inayowakabili ya kusafirisha wagonjwa.

Akitoa ombi hilo katika kikao cha baraza la madiwani la manispaa hiyo Naibu Meya, Shadida Ndile (CCM), amesema wabunge hao wakishirikiana wanaweza kutatua tatizo hilo ambalo kwa sasa limekuwa kubwa.

Amesema kuwa endapo manispaa hiyo ikipata gari la wagonjwa itasaidia kutatua changamoto ya usafiri kwa wagonjwa inayowakabili kwa Muda mrefu.

“Kwakweli manispaa yetu haina gari la kubebea wagonjwa hivyo tupambane kwa umoja wetu ili manispaa yetu iweze kupata gari hiyo itakayotusaidia kupunguza changamoto tuliyonayo hasa tunapopata mgonjwa anaetakiwa kuwahishwa kwenye matibabu” amesema Ndile.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles