29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Madee kumpa uhuru mwanawe

Glory Mlay

MWANAMUZIKI wa bongo fleva, Hamad Ally ‘Madee’ amesema iwapo mwanawe wa kike, Aimal Hamad, atachagua kuwa msanii litakuwa ni jambo la kawaida.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Madee alisema kuwa atamruhusu kufanya muziki kwasababu hata yeye amefuata nyayo za baba yake katika fani hiyo.

Alisema licha ya kuwepo kwa changamoto nyingi kwenye Sanaa kwa wanawake lakini hana budi kumruhusu kuonyesha kipaji chake kwa kuwa kila mtu amepangiwa ridhiki yake.

“Wazazi wanashauriwa kuwaangalia watoto wao wafanye kitu wanachotaka, hivyo siwezi kumpangia mtoto wangu  kitu cha kufanya katika maisha yake, akitaka muziki sawa, akitaka kuwa yeyote ni yeye na maisha yake,” alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles