29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Madam Rita: Bongo Star Search haijafa

Rita Paulsen
Rita Paulsen

NA WINFRIDA NGONYANI,

MKURUGENZI wa Benchmark Production, Rita Paulsen, ametolea ufafanuzi kuhusiana na mchakato wa kusaka waimbaji chipukizi katika shindano lake maarufu la ‘Bongo Star Search’ linalofanyika kila mwaka.

Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Rita kutambulisha kipindi chake kipya cha televisheni cha ‘Rita Paulsen Show’ kinachorushwa kila Jumapili katika runinga ya Azam two.

“Rita Paulsen Show ni kitu ambacho kimekuwa katika mawazo yangu zaidi ya miaka saba nyuma, kwa hiyo ni cha siku nyingi ni mipango ambayo nilikuwa nayo na sasa imetimia na ni moja tu ya mambo ambayo yapo pamoja na Bongo Star Search,” alisema.

Rita aliongeza kuwa, Bongo Star Search iko palepale na kuwatoa hofu Watanzania, huku akisema mazungumzo baina yake na uongozi wa Azam Tv yanaendelea kuona uwezekano wa kurusha matangazo ya kipindi hicho.

Kipindi cha Rita Paulsen Show ni kipindi cha kijamii chenye vipengele vya kuelimisha na kuburudisha familia.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles