24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Madaktari nchini India watoa visu 40 kwenye tumbo la mtu

Visu
Visu vilivyotoka tumboni

 

Katika mazingira yakutatanisha, madaktari nchini India katika mji wa Amristar wamefanikiwa kutoa visu 40 kutoka kwenye tumbo la mtu wakati wa upasuaji.

Mwanamume huyo (42), alimeza visu hivyo 40 ndani ya miezi mitatu, huku ikiwa bado haijafahamika kusudi lake lilikuwa nini.

Kwa mujibu wa Daktari Jatinder Malholtra, mwanamume huyo hakuwa amewaeleza madaktari juu ya tatizo lake.

“Baada ya vipimo, tuliligundua hilo na ndio tukafanya upasuaji japo ulikuwa ni upasuaji wa aina yake,” alisema Dk. Malholtra

Dk. Malholtra anasema, upasuaji huo ulifanywa na madaktari wapatao watano, ulifanyika kwa takribani saa tano na mgonjwa sasa yupo salama.

“Bado yuko chini ya uangalizi na pia tunatafuta sababu ya kumeza visu hivyo lakini tunaamini kwa kiasi kikubwa kuwa hili ni swala zima linalohusika na matatizo ya kisaikolojia. Na cha ajabu zaidi hata familia yake hawakulikulifahamu jambo hilo,” alisema Dk. Malholtra

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles