25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Mabasi ya mwendo kasi tishio biashara ya daladala

Mabasi ya mwendo kasiAsifiwe George na Ruth Mnkeni, Dar es Salaam

KUANZA rasmi kwa mabasi ya mwendo wa haraka Dar es Salaam huenda kukawa  tishio la biashara kwa wenye wamiliki wa daladala, imeelezwa.

Hali hiyo ilijitokeza jana baada ya abiria wanaotumia barabara ya Morogoro kutokea Kimara hadi Kivukoni kujitokeza kwa wingi kutumia mabasi hayo yalipoingia barabarani kwa mara ya kwanza huku yakitoa huduma ya bure ambayo itaendelea leo.

Baadhi ya madereva wa daladala wanaofanya safari kati ya Kimara na Posta na Mbezi hadi Kivukoni, walisema magari hayo huenda yakawakosesha hesabu za kupeleka kwa mabosi wao kwa kuwa abiria wengi huyakimbilia.

Mmoja wa madereva wa daladala, Juma Abdalla alisema kitendo cha mabasi hayo kutoa huduma bure kuanzia saa 4.00 asubuhi jana kitawasababishia hasara kubwa kwa sababu hawatarajii kufikisha kiwango cha fedha walichotakiwa kupeleka kwa mabosi wao.

“Leo (jana) tutapata hasara kubwa kwa sababu hatutafikisha kiwango cha fedha tunachotakiwa kukipeleka kwa mabosi wetu ukizingatia kwamba huduma hiyo inatolewa bure leo (jana) na kesho (leo),” alisema Abdalla.

Pamoja na malalamiko hayo,  wananchi  walieleza kuridhishwa na viwango vya nauli viliyopangwa na Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), huku wakisema wataokoa muda   kwa kuwa watafika mapema katika shughuli zao za uchumi.

“Pia ingekuwa vema magari haya yaanze kufanya kazi saa 11:00 asubuhi hasi saa 6:00 usiku ili kuondokana na usumbufu wa usafiri,” alisema.

Neema Salimu mkazi wa Kinondoni, alisema magari hayo yamekuwa mkombozi mkubwa kwake kwa sababu anafanya kazi Mbezi Mwisho na alikuwa akilazimika kutumia magari mawili hadi matatu kufika kazini.

Hata hivyo mbali na pongezi hizo, wananchi hao wamelalamikia tiketi za kuingilia kwenye vituo kwamba zinachukua dakika 10 kwa mtu mmoja kuruhusu kuingia kituoni jambo ambalo linapoteza muda mrefu.

Dereva Dotto Edward aliyekuwa akiendesha  basi namba T 144 BGV alisema gari hilo limeboreshwa miundombinu kwa sababu lina viti maalumu kwa ajili ya walemavu wa aina zote pamoja na wajawazito.

Alisema mtu yeyote anaweza kukaa katika viti hivyo, lakini anapopakia mlemavu au mjamzito anapaswa kumpisha.

 

VITUKO

Baadhi ya wanafunzi wa darasa la pili waliangua kilio baada ya basi walilokuwa wamepanda kupita kwenye kituo chao bila kusimama. Hiyo lilitokana na wanafunzi hao kutoelewa namna ya kutumia mashine zilizo ndani ya basi hilo ambazo humuarifu dereva kusimamisha gari.

 

MENEJA UDAT

Meneja Uhusiano wa UDART, Deus Bugaywa alisema changamoto kubwa waliyokumbana nayo kipindi hiki cha kuanza kwa mradi ni watu, pikipiki, bajaji na maguta  kuendelea kupita katika barabara za mabasi hayo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles