23 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

MAASKOFU 27 KKKT WATOA WARAKA MZITO


Na MWANDISHI WETU    |

BARAZA la Maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), limetoa waraka mzito unaochambua masuala ya jamii, uchumi, maisha ya siasa, umuhimu wa Katiba Mpya na matukio yaliyo kinyume na tunu na misingi ya taifa.

Waraka wa baraza hilo linaloundwa na idadi ya maaskofu 27, akiwamo Askofu Mkuu wa KKKT, Dk. Fredrick Shoo, ulianza kusambaa katika mitandao ya kijamii jana asubuhi na umekusudiwa kusomwa leo na wiki ijayo katika makanisa yote ya KKKT hapa nchini.

Mmoja wa watumishi wa KKKT na askofu ambaye hakutaka jina lake kuandikwa gazetini, alithibitisha kwamba waraka ulioonekana jana katika mitandao ya kijamii ndio ulioandaliwa na baraza hilo.

Pia waliliambia MTANZANIA Jumapili kwa nyakati tofauti kuwa hadi jana waraka huo ulikuwa tayari umesambazwa kwa maaskofu na wachungaji wote wa kanisa hilo nchini na ulitarajiwa kusomwa leo.

MTANZANIA Jumapili lilipomuuliza Askofu Shoo kwa simu jana kama ni kweli baraza hilo liliandaa waraka huo ulioonekana katika mitandao ya kijamii, alishindwa …

Kwa habari zaidi jipatie nakala yako ya gazeti la MTANZANIA. 
- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles