24.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Lyon wajiondoa kwa Adebayor  

adebayorLYON, ITALIA

KLABU  ya  Lyon imejiondoa katika mipango  ya  kumsajili aliyekuwa mshambuliaji wa  timu ya  Arsenal, Manchester City na Tottenham,  Emmanuel Adebayor (32).

Adebayor ambaye ni mchezaji huru  baada ya kumaliza  mkataba  wake  na klabu ya  Crystal Palace, alikuwa mbioni kujiunga na timu ya  Lyon.

Nyota huyo wa Togo, Ijumaa iliyopita alikuwa jijini Lyon, Ufaransa kwa ajili ya mazungumzo na  kocha wa Lyon, Bruno Genesio.

Lakini klabu hiyo  haikukubaliana na nyota huyo  kutokana na umri wake kuwa mkubwa,  huku ikidai kwamba   atashindwa kuwa na msaada katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ambayo timu hiyo inashiriki msimu huu.

Klabu hiyo  inayoshiriki Ligi Kuu  ya Ufaransa  (Ligue 1), pia ilidai  haitafurahishwa  na hatua za kumkosa mchezaji huyo kwa miezi miwili ya msimu huu  wakati  akiwa na  timu yake ya taifa  katika Kombe la Mataifa  barani Afrika.

Katika hatua nyingine, Lyon ilisema ina furaha kumsajili mshambuliaji mwengine,  Jean Phillipe Mateta, baada ya Adebayor kusema kuwa angependa kuliwakilisha taifa lake katika kombe la bara Afrika mapema 2017, hatua ambayo ingemfanya kutochezea timu hiyo kati ya mwezi mmoja hadi miwili.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles