Na BRIGHITER MASAKI-DAR ES SALAAM
MSANII wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka sababu ya kumtoa mdogo wake Erick kwenye mitandao ya kijamii.
Msanii huyo amedai mdogo wake bado ana umri mdogo, hivyo hawezi kumlazimisha kuja kuwa staa, ila akikua ataamua nini akifanye, lakini kuanza kumuingiza kwenye mitandao kwa sasa ni makosa.
Akizungumza na MTANZANIA jana, amesema alifanya makosa makubwa kumuweka mitandaoni itakuwa kama anamlazimisha kufanya atakalo yeye.
“Nimejifunza kitu katika maisha kuwa, kila mtu na maisha yake hivyo ni vyema nikamuweka nje ya mitandao hadi pale mwenyewe atakapoamua, kwanza ni mwanafunzi yupo darasa la sita anakaribia kumaliza la saba ana miaka 12.
“Nikimuweka sana naweza nikawa naingilia uhuru wake hapo badae anaweza asifurahie kuwa kwenye mitandao, hivyo nimemwondoa ili nisimchagulie maisha ya kuishi na vitu vya kufanya, ila hapo baadae akihitaji basi nitamuunga mkono,”alisema Lulu.