27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

LUKUVI: KIGWANGALLA HAJANISHIRIKISHA MGOGORO WA KIWANJA ARUSHA


Na MWANDISHI WETU-DODOMA -

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, amesema Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kigwangalla, hakumuuliza kuhusu suala la kiwanja namba 4091 kilichoko Njiro jijini Arusha, alichodai kilivamiwa na watu, akiwamo mmoja wa mawaziri wakuu ambaye hakumtaja jina moja kwa moja na kujenga nyumba za makazi.

Januari 31, mwaka huu, Dk. Kigwangalla, alitangaza notisi ya siku 30 kwa watu waliovamia kiwanja hicho chenye ukubwa wa heka 20.215, kuwasilisha nyaraka za umiliki pamoja na vibali vya ujenzi kwa Kamishna wa Ardhi.

Notisi hiyo pia iliwataka wavamizi wa kiwanja hicho alichosema kinamilikiwa na Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro, kuambatanisha barua yenye maelekezo kwa nini majengo hayo yasivunjwe kupisha uendelezaji wa mradi wa taasisi ya Serikali.

Aidha, katika moja ya kauli zake, Dk. Kigwangalla, alisema Wizara ya Ardhi inafanya uhakiki ili ……

Kwa habari zaidi jipatie nakala yako ya gazeti la MTANZANIA.
- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles