23.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Lugola: Hakuna ugaidi

 Nora Damian, Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amesema Watanzania wasiwe na hofu juu ya tishio la ugaidi kwani nchi ina usalama wa hali ya juu.

Akizungumza leo Juni 20, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wakimbizi Duniani, amesema vyombo vya ulinzi vinaendelea na uchunguzi juu ya suala hilo.

“Serikali iko imara na vyombo vya ulinzi na usalama viko imara vimejipanga vizuri kwa jambo au tishio lolote la usalama.

“Tahadhari ambayo imetolewa na wenzetu wa Marekani hizi ni sehemu ya taarifa za kawaida na tumeweza kuwasiliana nao kupitia jeshi la polisi.

“Watanzania wasiwe na hofu wala wasiwasi nchi iko imara  ina usalama wa hali ya juu na vyombo vinaendelea kufanya kazi yake,” amesema Lugola.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles