25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

LISSU AWAPA SOMO MAWAKILI WAPYA

RAIS wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu

Na ASHA BANI-DAR ES SALAAM

RAIS wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu amesema kwa kipindi cha sasa mawakili na wanasheria wanatakiwa kujitokeza na kuielekeza jamii njia sahihi ya kufuata ikiwamo utawala wa sheria.

Pia amewataka wanasheria hao kuungana   kutetea chama chao kwa sababu  itakuwa nchi ya kwanza duniani kufutwa   chama cha aina hiyo.

Alikuwa akizungumza jana baada ya Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahimu Juma kuwaapisha mawakili wapya 248 katika viwanja vya Mahakama Kuu  Dar es Salaam.

Alisema mawakili wanatakiwa kujitokeza kuilekeza jamii njia sahihi ya kufuata ikiwamo utawala wa sheria haki za binadamu na demokrasia kutokana na mazingira ya sasa.

“TLS inakabiliwa na tishio kubwa la kufutwa lakini itakuwa ni nchi ya kwanza kufuta chama cha mawakili  jambo ambalo litashangaliwa na wengi kwa vile  sisi ni watu muhimu katika taifa,’’ alisema Lissu..

Alisema  mawakili hao 248 walioapishwa  jana ukiwajumlisha wote unapata idadi ya mawakili  6,329 hivyo kuna uwezekano mkubwa wa kuongezeka  huduma za uwakili na sheria.

Lissu alisema  Tanzania ipo katika nafasi nzuri ya pili kwa uwingi wa wanasheria Afrika Mashariki,  ya kwanza ikiwa  Uganda  hivyo hali siyo mbaya kama nchi.

Naye Kaimu Jaji Mkuu, Profesa Ibrahimu Juma alisema mawakili ni watu muhimu   na anaamini kwa idadi hiyo kazi zitafanyika kwa uelewa na weledi katika mahakama .

“Mawakili Tanzania wengi wao ni vijana wadogo  hivyo wanatakiwa kujiendeleza kusoma kwa sababu wanasheria   wanaosoma sasa ni tofauti na waliopata elimu hiyo zamani.

“Muitumie nafasi hii katika kuelewa shughuli mbalimbali za  mahakama kwa haki muwe wanasheria wazuri wa kusaidia nchi hata kwenye mambo mbalimbali ya  sheria  yakiwamo ya  uchumi na  mataifa,” alisema Profesa Juma.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles