23.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Lady Gaga aachana na mchumba wake

Lady Gaga
Lady Gaga

NEW YORK, MAREKANI,

MWANAMUZIKI na mwigizaji mashuhuri nchini Marekani Lady Gaga, amefichua kwamba yeye na mchumba wake Taylor Kinney wameachana kwa muda na kwamba wanaweza kurudiana baadaye.

Lady Gaga na Kinney wamekuwa pamoja kwenye uhusiano kwa miaka mitano, lakini taarifa ya wawili hao kutengana zilienea muda mrefu kabla ya Gaga kuthibitisha kupitia ukurasa wake wa Instagram.

“Bado tunapendana sana lakini ndoto zetu za kuwa pamoja kimaisha zinaonekana kuwa ngumu, kila mmoja ana shughuli zake na tulikuwa hatuishi nyumba moja, hilo ni tatizo,” aliandika Gaga.

Uhusiano wa wawili hao ulianza mwaka 2011 na suala la uchumba lilianza rasmi katika Sikukuu ya Wapendanao ya mwaka 2015 – Februali 14.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles