27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Kura ya Bunge Brexit kufanyika Januari 15

LONDON, UINGEREZA

UPIGAJI kura bungeni kuhusu makubaliano na Umoja wa Ulaya (EU) juu ya mchakato wa Uingereza kujiondoa rasmi kutoka umoja huo, maarufu kama Brexit utafanyika Jumanne ijayo.

Awali mwezi uliopita Waziri Mkuu wa Uingereza, Theresa May alilazimika kuahirisha kura hiyo baada ya kukiri kuwa mpango wake huo ungeshindwa.

Licha ya kutangaza mchakato huo, May alisema Uingereza itajikuta mahali pagumu iwapo mpango wake na Ulaya utakataliwa.

Hadi sasa dalili zinaonesha hajaweza kuwashawishi wabunge wenye msimamo mkali kuunga mkono mpango wake.

Uingereza inatarajiwa kuondoka rasmi kutoka Umoja wa Ulaya Machi 29 mwaka huu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles