Na Nora Damian
Wakati uchaguzi ukiendelea katika mkutano mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) upande wa Profesa Ibrahim Lipumba, vimeokotwa vipeperushi ndani ya ukumbi vyenye majina ya watu wanaodaiwa kuwa ndio wanaopaswa kuchaguliwa.
Zoezi la uchaguzi linaendelea katika ukumbi wa Lekam Buguruni na tayari wajumbe wamepiga kura kumchagua mwenyekiti na makamu mwenyekiti kwa upande wa Zanzibar.
Mmoja wa viongozi wa Kamati ya Uchaguzi aliwaonyesha wajumbe mojawapo ya kipeperushi kilichookotwa na kusema kuwa ni feki hivyo kipuuzwe.
“Kamati ya Uchaguzi haijaandaa kitu kama hiki, ieleweke vipeperushi hivi ni feki na hatuhusiki navyo kama kamati,” amesema kiongozi huyo.