IKIWA ni mechi nne tu zimechezwa msimu huu, Verona ya Ligi Kuu ya Italia (Serie A) imemfukuza kazi kocha wake, Eusebio Di Francesco.
Di Francesco (52), amefukuzwa baada ya Verona kufungwa bao 1-0 na Bologna, matokeo yanayoiacha ikiwa mkiani mwa msimamo.
“Hellas Verona FC inatangaza kusitisha majukumu ya Eusebio Di Fransesco kama mkuu wa benchi la ufundi,” imesomeka taarifa ya Verona.
Kocha huyo aliajiriwa majira ya kiangazi, mwaka huu, kuchukua nafasi ya Ivan Juric aliyetimkia Torino.