31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Kiongozi wa upinzani Malaysia akamatwa kwa ufisadi

KUALA LUMPUR, MALAYSIA

KIONGOZI wa upinzani wa Malaysia na Naibu Waziri Mkuu wa zamani Ahmad Zahid Hamidi alikamatwa jana na maofisa wa Tume ya Kupambana na Ufisadi.

Kukamatwa kwa Zahid Hamidi kunatokana na  uchunguzi wa matumizi mabaya ya mamlaka, kuvunja uaminifu, na kushiriki utakatishaji wa fedha kupitia wakfu unaohusishwa na familia yake.

Tume hiyo imesema Hamidi atafikishwa mahakamani leo kwa mujibu wa  sheria za kukabiliana na ufisadi na utakatishaji wa fedha.

Hamidi  kiongozi wa chama cha upinzani cha Malay ni miongoni mwa viongozi wa ngazi ya juu kukamatwa baada ya Waziri Mkuu wa zamani, Najib Razak na mke wake, kukamatwa kwa madai kama hayo baada ya kushindwa katika uchaguzi wa Mei.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles