24.4 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

KIGWANGALLA AMPA MTIHANI MGANGA MKUU PWANI

NA GUSTAPHU HAULE

-Kibaha

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla, amemtaka Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Beatrice Byalugaba atumie timu ya wataalum   kufuatilia huduma ya upasuaji   katika vituo vya afya na hospitali mkoani humo  ziwe katika viwango vinavyohitajika.

Pia ametoa miezi mitatu kwa mganga huyo kuhakikisha anasimamia marekebisho ya chumba cha upasuaji   katika kituo hicho   wananchi wanaotumia kituo hicho waweze kupata huduma bora.

Dk. Kigwangala  alitoa kauli hiyo jana mjini Kibaha alipopokea vifaa tiba 831 vyenye thamani zaidi ya milioni 400 vilivyotolewa na Mbunge wa   Kibaha Mjini Silvestry Koka (CCM).

Vifaa hivyo ni kwa ajili ya kuboresha huduma ya afya nchini hususan kwa  vituo vya afya, zahanati na hospitali za Jimbo la Kibaha Mjini

Alisema   kazi ya Mganga Mkuu ni kusimamia utekelezaji wa shughuli zote za huduma ya afya    katika mkoa wake hivyo ni jukumu lake  kuhakikisha maagizo yote yanayotolewa na Serikali yanafanyiwa kazi kwa wakati.

“Nimepita katika chumba cha upasuaji katika kituo hiki cha afya lakini yapo marekebisho madogo yanahitaji kufanyiwa kazi hivyo Mganga Mkuu nakupa miezi mitatu ya kufanya maboresho katika theatre hii iweze kufikia viwango,” alisema Kigwangala.

Alisema marekebisho hayo yafanyike katika vituo vyote vya afya na hospitali za Mkoa wa Pwani  kuepusha madhara kwa wagonjwa wanaofuata huduma hiyo na hata wahudumu ambao wamekuwa wakitoa huduma ya upasuaji katika maeneo yao.

Mbunge wa Kibaha Mjini,  Silvestry Koka (CCM), alisema   vifaa hivyo vina thamani  zaidi ya Sh milioni 400 ambavyo vitagawiwa katika vituo vya afya na zahanati   katika jimbo lake na hata mikoa mingine   itakapobidi.

Koka alisema   mchakato wa kuagiza vifaa hivyo ulianza   mwaka 2011 kwa kutoa Sh milioni 12 kwa ajili ya kuwaleta wataalamu kutoka Marekani kupitia Kampuni ya Project Cure.

Wataalamu hao walifanya uchunguzi   kujua mahitaji katika vituo vya afya, zahanati na hospitali.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles