24.4 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

KESI YA BILIONEA MSUYA: JAMHURI YAKATA RUFAA KUPINGA USHAHIDI KWA NJIA YA MDOMO

Na UPENDO MOSHA -MOSHI


UPANDE wa Jamuhuri katika kesi ya msingi ya mauaji ya mfanyabishara, bilionea Erasto Msuya umekata rufaa juu ya uamuzi wa mahakama  wa kukataa ushahidi wa maelezo yaliyotolewa kwa mdomo na shahidi wa tisa.

Hatua hiyo inatokana na  uamuzi wa  Mahakama dhidi ya shahidi namba tisa, Inspekta, Samuel Maimu, ambako upande wa Jamhuri haukuridhika na uamuzi wa Mahakama uliotolewa awali. 

Mahakama ilitoa uamuzi wa kukataa ushahidi uliowasilishwa kwa njia ya mdomo mara mbili na shahidi huyo, baada ya mawakili wa upande wa utetezi wakiongozwa na Wakili Majura Magafu, kuwasilisha pingamizi la kukataa ushahidi huo kwa vile  ni kinyume cha sheria. 

Wakiwasilisha   hati ya kuomba kukata rufaa, mawakili wa upande wa Jamuhuri wakiongozwa na Wakili Omari Kibwana, walisema wameamua kupeleka hati ya kukata rufaa dhidi ya ushahidi uliowasilishwa kwa njia ya mdomo.

Kabla ya kuibuka  malumbano ya sheria baina ya mawakili wa upande wa utetezi na Jamhuri, shahidi huyo  akiongozwa na wakili wa upande wa Jamhuri, Abdala Chavula, alidai kuwa Agosti 13 mwaka 2013 mtuhumiwa namba tano alikiri kuhusika katika mauaji ya mfanyabiashara huyo. 

Sehemu ya mahojiano ilikuwa hivi:

Wakili: Shahidi, ebu ieleze mahakama hii Agosti 13 mwaka 2013 wakati ukizungumza na mtuhumiwa alikueleza nini?

Shahidi:  Alieleza kuwa yeye ndiye aliyekuwa amekamata bunduki na kumuua Erasto Msuya.

 Wakili: Je siku iliyofuata baada ya kumuhoji mtuhumiwa nini kiliendelea?

Shahidi: Baada ya kumkamata tulifunga safari siku inayofuata kuja Kilimanjaro. 

Wakili: Nini kilijiri ulipofika Kilimanjaro?

Shahidi: Tulimpeleka kwa mkuu wa upelelezi Mkoa wa Kilimanjaro wakati huo alikuwa ni Ramadhani Nganzi  na pia mtuhumiwa alikiri kweli kuhusika na mauaji ya Msuya. 

Wakili: Maneno hayo aliyasema wapi na nani ulikuwa naye.

Shahidi: Aliyasema maneno hayo kwa RCO na mimi pia nilikuwapo nikisikia akiongea na pia tulikuwa na askari, Koplo Atwai ambaye tulikuwa naye safarini kurudi Kilimanjaro.

 

Wakili:Baada ya kueleza nini kilifuata?

Shahidi : Afande RCO  alitoa maagizo kwamba tumpeleke kwa mlinzi wa amani na baadaye aliwekwa mahabusu kwa ulinzi. 

Wakili: Jana ulisema kule mlikuwa na watuhumiwa wawili. Je mwingine mlimuacha wapi mkiwa kule Tabora ?

Shahidi: Mtuhumiwa mwingine ambaye ni Sadiki alikuwa kwenye gari. 

Wakili: Eneo mlilokuwa wakati huo ni eneo gani

Shahidi: Kijiji cha Rimbura

 Wakili: Na baadaye mlimpeleka wapi?

Shahidi: Tulimpeleka mpaka Kituo cha Polisi Kaliuwo. 

Wakili: Baada ya kufika kituo cha polisi Kaliuwo nini kiliendelea kwa Sadiki?

Shahidi : Aliwekwa mahabusu mpaka kesho yake 

Wakili: Nini kilitokea?

Shahidi:Alisema anataka kwenda Limbula kuna vitu aliviacha, tulienda lakini sikuona fedha na baada ya kutoka Lembula na kufanya upekeuzi hatukuona kitu chochote. Tulirudi nayee tena kituoni na baada ya kufika waliandika tena maelezo yao.

 

Wakili: Shahidi ebu eleza uhusika wa mtuhumiwa namba sita ulikuwa vipi?

Shahdi: Alisema siku ya tukio alikuwa na pikipiki moja na walikuwa maeneo ya Mjohoroni Bomang’ombe  na walikuwa wakiangalia kama kuna dharura waweze kumsaidia Karimu na baada ya mauaji  waliondoka na pikipiki. 

Upande wa utetezi ukiongozwa na Magafu ulisema: “Tunashikitishwa kuona upande wa mashtaka wanatumia sheria vibaya kwa kuwaadhibu watuhumiwa kuendelea kukaa ndani  kwa sababu kila hatua tunayopiga wao wanakimbilia kukata rufaa  ili tu kesi isimame.  Ni kweli kukata rufaa ni haki yao kisheria lakini ni kwa sababu tu za msingi  sisi hatujafurahishwa na jambo hilo.

Kesi hiyo ya mauji ya Mfanyabiashara wa Madini, Erasto Msuya yaliyotokea Julai 7 mwaka 2013, itaendelea kusikilizwa katika  Mahakama Kuu Kanda ya Moshi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles