27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Kenya na Uganda zakabiliwa na tatizo la kitaifa la kusambaza umeme

NAIROBI, KENYA 

MATAIFA ya Afrika Mashariki ya Kenya na Uganda yanakabiliwa na tatizo la kitaifa la kukatika kwa umeme.

Kupitia mtandao wa Twitter, Shirika la Umeme la Kenya, Power and Lighting, limesema kuwa limepoteza uwezo wa kusambaza umeme kwenye gridi ya taifa kutokana na matatizo katika mfumo wake.

Katika taifa jirani la Uganda, hali ni kama hiyo hiyo baada ya shirika la kusambaza umeme, UETCL, pia kutangaza tatizo la kitaifa la kusambazwa kwa nguvu za umeme jana asubuhi.

Katika taarifa, kampuni ya Umeme Limited inayopata umeme wake kutoka kwa shirika la UETCL, imesema kuwa maofisa wa shirika hilo wanashughulikia tatizo hilo kuhakikisha limerekebishwa mara moja. 

Bado haijabainika iwapo matatizo hayo katika mataifa hayo mawili yanaingiliana.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles