31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Kendrick Lamar akanusha kuondoka TDE

 CALIFORNIA, MAREKANI 

STAA wa muziki wa hip hop nchini Marekani, Kendrick Lamar, amekanusha taarifa kuwa ameondoka kwenye lebo ya TDE. 

Msanii huyo ambaye ametamba na nyimbo mbalimbali kama vile King Kunta, Swimming Pool, Humble Bitch Don’t Kill My Vibe, miezi ya hivi karibuni amekuwa akihusishwa kuondoka kwenye lebo hiyo baada ya kimya cha muda mrefu. 

Lakini Lamar amesema hakuna ukweli wowote juu ya taarifa hizo na hajui wapi zinakotoka, bado ataendelea kuwa hapo na kuna kazi mpya zinakuja siku za hivi karibuni. 

“Nani anajua habari zangu nyingi kuliko mimi mwenyewe? Nimekuwa nikizisikia kutoka sehemu mbalimbali na zinanishangaza, ukweli ni kwamba nimechoshwa na hali hii, bado nitaendelea kuwa TDE na kuna kazi mpya zipo njiani,” alisema msanii huyo. 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles