23.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Katibu Mkuu Mambo ya Nje atoboa siri watendaji wizara hiyo kubweteka

Mwandishi Wetu, Dar es Salaam



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Faraji Mnyepe amesema watendaji katika wizara hiyo wamezoea kufanya kazi kwa mazoea kuwa kituo cha kufanyia kazi ni nje ya nchi.

Dk. Mnyepe amesema hayo leo Jumatano Oktoba 3, Ikulu jijini Dar es Salaam, muda mfupi baada ya kuapishwa na Rais John Magufuli, kuwa Katibu Mkuu katika wizara hiyo.

“Nikutoe hofu Mheshimiwa Rais, nakwenda kufanya kazi sina wasiwasi na idhini yako uliyonipa nikafanye kazi. Nilisikia ulipomuapisha Naibu Waziri (Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Damas Ndumbaro) ulisema wazi wizara hiyo haifuraishi.

“Ulitoa sababu na sababu zile ni za kweli zote. Matatizo ya wizara yako mengi lakini katika salamu zangu hizi naomba niyakweke katika sehemu mbili, ya kwanza barua kwa nini hazijibiwi.

“Mentality (dhana) au culture (utamaduni) ni kwamba ukishaajiriwa katika wizara ile kituo chako cha kazi ni nje ya nchi, kwa hiyo mtu ukishateuliwa ukirudishwa unarudishwa ili utafutiwe kituo kingine cha kazi, hiyo ndiyo mentality.

“Kuna makundi katika wizara ile kama ulivyoanisha siku ile, mengi sana… Mheshimiwa rais naenda kuishi katika kiapo changu,” amesema Dk. Mnyepe.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles