33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Kansela Merkel atunukiwa shahada ya udaktari

NEW YORK, MAREKANI

KIONGOZI wa serikali ya Ujerumani, Kansela Angela Merkel, ametunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima ya Chuo Kikuu maarufu cha Harvard. Rais wa Chuo cha Havard, Larry Bacow, aliyemtunukia Merkel tuzo hiyo amemueleza Kansela huyo wa Ujerumani kama mwanasiasa mwenye nguvu barani Ulaya. 

Taarifa ya chuo hicho imemwelezea Merkel kwa matamshi yake kwa kusimama kidete wakati wa mgogoro wa wakimbizi ulioanza mwaka 2015 nchini Ujerumani, wakati aliporuhusu idadi kubwa ya wakimbizi na kukabiliwa na ukosoaji mkubwa nchini mwake. 

Kwenye hotuba yake kwa wanafunzi, wakati wa mahafali ya 368 ya chuo hicho cha Havard, Merkel aliwaonya wanafunzi dhidi ya kuchanganyikiwa na kuchukulia uongo kuwa ukweli na ukweli kuwa ni uongo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles