24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

KAMPUNI YATAKIWA KUKAMILISHA BARABARA YA JUU

Na ESTHER MNYIKA-DAR ES SALAAM

SERIKALI imeitaka Kampuni ya M/s China Civil Engineering Construction Corparation (CCECC) kukamilisha mradi  wa ujenzi wa barabara za juu  ‘interchange’ katika makutano ya Ubungo ndani ya miaka ya mitatu.

 Mkataba uliofikiwa unamtaka Mkandarasi ambayo ni Kampuni ya CCECC kutoka China kuanza ujenzi huo mara moja na ujenzi huo ambao unatarajiwa kutumia takriban miezi 30  kukamilika  

Mtendaji Mkuu  wa Wakala wa Barabara Tanzania  (TANROADS), Patrick Mfugale aliyesema hayo Dar es Salaam jana baada ya kusaini mkataba na kampuni hiyo ya  ujenzi wa barabara za juu   katika makutano ya Barabara ya Sam Najoma, Morogoro na Mandela.

“Zaidi ya Sh bilioni 177.4 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi huo ambao utakawekewa jiwe la msingi Machi mwaka huu.

“Hakikisheni mnaanza ujenzi mara moja kwa sababu Serikali imeshakamilisha taratibu zote na tayari Sh bilioni 2.1 zimelipwa kwa ajili ya fidia kwa wananchi walioguswa na mradi huo,”  alisema Mfugale.

Alisema ujenzi wa Ubungo interchange unatekelezwa  kwa fedha ya mkopo kutoka Benki ya Dunia  kwa ajili ya   uboreshaji miundombinu ya usafiri Dar es Salaam.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles