Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Sukari ya Kilombero, Guy Williams (wa pili kulia) akipokea cheti cha shukrani (Certificate of Appreciation) kwa udhamini wao wa Tuzo za Consumer Choice Africa zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital
Kama mzalishaji mkubwa wa sukari nchini Tanzania, Kampuni ya Sukari ya Kilombero (KSCL) iliungana na watumiaji kutambua chapa na watu bora kwa kudhamini Tuzo za Consumer Choice Africa.
Baada ya mchakato wa kupiga kura, hafla ya kukabidhi tuzo hizo ilifanyika Novemba 12, 2022 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Sukari ya Kilombero, Guy Williams (kushoto) akikabidhi tuzo kwa mwakilishi kutoka Halotel wakati wa hafla ya Tuzo za Consumer Choice Africa.Mkuu wa idara ya Mahusiano wa Kampuni ya Sukari ya Kilombero, Ephraim Mafuru akijiandaa kukabidhi tuzo kwa baadhi ya washindi katika hafla hiyo.Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Sukari ya Kilombero, Guy Williams akitangaza washindi katika baadhi ya vipengele kwenye hafla ya Tuzo za Consumer Choice Africa.Timu ya mauzo kutoka Kampuni ya Sukari ya Kilombero (KSCL) wakionyesha bidhaa za Bwana Sukari katika hafla hiyo.