23.3 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Kaka wa Nicki Minaj kwenda jela maisha

New york, Marekani

KAKA wa rapa Nicki Minaj, Jelani Maraj, anaweza kwenda jela miaka 25 au maisha kutokana na tuhuma za ubakaji za mwaka 2015.

Maraji mwenye umri wa miaka 41, alianza kufikishwa mahakamani mwaka 2017, akidaiwa kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 11. Hiyo sio mara yake ya kwanza kukutwa na kashfa kama hiyo, aliwahi kutuhumiwa kumbaka mtoto wake wa kufikia.

Wiki tatu zilizopita Nicki Minaj alijaribu kupambana ili kuweza kulimaliza suala hilo, lakini inaonekana kugonga mwamba.

Nicki Minaj aliwahi kumuwekea dhamani ya dola 100,000, ambazo ni zaidi ya milioni 229 za Kitanzania, lakini baada ya hapo Nicki hakuwa na msaada mwingine wa kumsaidia kaka yake baada ya kugundua kuwa anahusika kwenye kesi hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles