30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

KAJALA MASANJA: NILINUSURIKA KIFO MARA MBILI

 

 

Na KYALAA SEHEYE, DAR ES SALAAM

STAA wa filamu za Bongo, Kajala Masanja, amesema aliwahi kunusurika kifo kutokana na kupata mshtuko mara mbili mara, baada ya kutoka selo alikokuwa akituhumiwa katika kesi ya kuuza nyumba kwa wizi.

Kajala alisema labda leo asingekuwa hai kama angeendelea kufuatilia matusi na lawama za mashabiki wake alizozikuta mitandaoni baada ya kutoka kwenye kesi hiyo.

“Sikuwa nikijua kinachoendelea huko mitandaoni, nilipotoka selo nikakutana na matusi ya kila namna, sikuweza kuyavumilia, wakati wote nilikuwa nikilia na kujutia kutoka selo, nilitamani hata nirudi huko lakini haikuwezekana.

“Kutokana na kuumia huko nikajikuta mara mbili tofauti nikizidiwa kwa kupata mshtuko wa moyo ambapo nilikimbizwa hospitali nikiwa sijitambui, nilitundikiwa chupa ya maji, lakini hali hiyo iliendelea hadi nilipokuja kuonyeshwa watu waliokuwa wakinitumia meseji hizo za matusi ndipo mapigo ya moyo yakarudi kawaida,” alieleza Kajala.

Kajala aliongeza kwamba alipogundua kwamba waliokuwa wakimtumia matusi kwenye mitandao ya jamii ni kikundi cha wasichana wanaofanya biashara ya miili yao na hajui kwanini walifanya hivyo, hapo ndipo alipoanza kuwa na moyo wa ujasiri akaanza kupuuza mambo ya mitandaoni.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles