24.5 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Kairuki avutiwa uwekezaji kiwanda cha kuku, kilimo

Na MWANDISHI WETU -IRINGA

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Angellah Kairuki amevutiwa na uzalishaji wa chakula cha kuku, ufugaji wa kuku pamoja na mbogamboga  katika Kongani ya Ihemi kwenye ushoroba  wa Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania (SAGCOT) na kusema kuwa uwekezaji huo unakwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kujenga uchumi wa kati na viwanda ifikapo mwaka 2015.

Hayo aliyasema jana mjini hapa baada ya kutembelea kwa nyakati tofauti viwanda vya Silverlands, Masifio Estates, Pyrethrum Tanzania (PCT), Qwihaya General Entreprises na Sao Hill.

Kairuki alisema kuwa uwekezaji wa kuku na kilimo cha mbogamboga  katika eneo hilo una mchango mkubwa katika  kuongeza kipato kwa wakazi wa Iringa.

“Nimevutiwa sana na uwekezaji huu wa kiwanda cha kutengeza chakula cha kuku, ufugaji wa kuku na kilimo cha mbogamboga. Kama Serikali tutaendelea kuboresha na kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji hapa nchini.

“Hii siyo hadithi,  nimejionea  mwenyewe  namna  uzalishaji  mkubwa wa kuku na mbogamboga unavyofanyika, na sisi kama  Serikali tutahakikisha  tunawaunga  mkono  ili kujenga na kuimarisha  sekta husika pamoja kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi  hapa nchini,” alisema Kairuki.

Alisema kiwanda cha  Silverlands kimekuwa chachu ya maendeleo kwa upande wa kuku,  lakini  pia wamekuwa  wanunuzi wakubwa wa  zao la mahindi kutoka kwa wakulima wa  mikoa ya Nyanda za Juu Kusini  na hivyo kuliongezea thamani zao hilo.

Kwa upande wake,  Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela alisema kuwa kiwanda cha Silverlands kimekuwa na mchango mkubwa na kuhakikisha maendeleo ya mkoa  huo kwa kuwahakikishia wakulima soko la uhakika la mazao ya mahindi na soya.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles